Thursday 12 April 2012

Kupatikana Kwa Chuma (Hadiyd, Iron) الحديد













Katika vitu vya kiasili ambavyo Qur’an imevielezea ni chuma (hadiyd au iron). Mwenyezi Mungu anatuambia katika Qur’an.
 
 “...Na tumeteremsha chuma chenye nguvu nyingi na manufaa kwa watu...” Qur’an 57:25
 
Wataalam wa lugha ya kiarabu wanalitafsiri neno Anzal kwa kusema kuwa ni “Kushushwa kwa kitu au kuletwa kwa kitu toka angani (Sent down). Je chuma (iron) ni madini ambayo ardhi yetu hii haiwezi kujitengenezea yenyewe? Jibu lake ni ndio. Chuma ni matokeo ya kupasuka pasuka kwa Nyota zilizoko angani, nyota ambazo ni kubwa sana kuliko Jua (sun) letu ili lililoko katika anga letu ili. Hali hiyo ya kutokea hayo mapande, yanayosababisha sisi wakazi wa dunia yetu kupata chuma, yanatokea baada ya nyota hizo kufikia hali ya uzee (Nova stage) kipindi ambacho joto katika nyota hizo hufikia nyuzi joto zinazo kadiriwa kuwa zaidi ya nyuzi digirii milioni mia moja. Wakati huo chuma kinakuwa kingi sana katika nyota hizo. Joto linapokithiri kwa kiwango hicho, nyota hizo zinashidwa kuvumilia na hapo ndipo zinapo pasuka mapande mapande, mapande hayo ambayo hutawanyika huku na huko na kuelekea mielekeo tofauti tofauti. Na hapo basi mapande mengine ndio huelekea huku katika dunia yetu. Na yanapokaribia anga la dunia yetu baadhi yake huvutwa na nguvu ya mvutano (gravitation force), na hii ni baada ya kupungua sana kwa ukubwa wake, na ni nadra sana mapande haya kushuka kwa ukubwa wa kuonekana. Bali mengi yao huja kwa mfumo wa kama vumbi. Na kupitiliza hadi chini ya ardhi na huko ndiko ujiunda pamoja na kujitengeneza majabali. Na sisi ndipo huwa rahisi kuchimba hicho chuma na kuki tenganisha na udongo na kupata chuma cha Pua. Chuma ambacho tunakitumia katika matumizi mbalimbali, kuanzia zana za kivita mpaka vifaa vya majumbani. Wataalamu wameligundua ili hivi karibuni tu, wakati Qur’an imekwisha lieleza miaka 1400 iliyopita.
Kitu kingine cha ajabu katika maandishi ya kiarabu, wao huipa thamani kila herufi iliyoko
katika maandishi yao. Mfano neno Bismillahi Al-Rahman Al-Rahim                                              
Bismillahi Al-Rahman Al-Rahim.
بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ
 
Thamani yake katika namba ni 786. Hili ni neno lenye herufi kumi na tisa sasa ni vipi thamani hiyo inapatikana, basi angalia jedwali hapa chini.


Table of Sequential & Gematrical Value of The Arabic Alphabet
Sequential Value
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
Arabic Letters
English
A
B
G
D
H
W
Z
HH
TT
Y
K
L
M
N
Gematrical Value
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
20
30
40
50
 
Sequential Value
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
Arabic Letters
ص
English
S
‘A
F
SS
Q
R
Sh
T
Th
Kh
Dh
DD
ZZ
Gh
Gematrical Value
60
70
80
90
100
200
300
400
500
600
700
800
900
1000
Baada ya kujua kila herufi ina thamani gani sasa basi hebu na tuangalie thamani ya neon Bismillahi Al-Rahman Al-Rahim. بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ (Bismi with Arabic text)


No.
Arabic
English
Letter Qntts
Arabic letter
Gematrical value
Total
1
Bismi
In the name of
3
بِسْمِ
2, 60, 40
102
2
Allah
God
4
اللَّهِ
1, 30, 30, 5
66
3
Al-Rahman
Most Gracious
6
الرَّحْمَـٰنِ
1, 30, 200, 8, 40, 50,
329
4
Al-Raheem
Most Merciful
6
الرَّحِيمِ
1, 30, 200, 8, 10, 40
289
TOTAL
19
١٩
786
 
Baada ya kuona thamani ya neno Bismillahi Al-Rahman Al-Rahim, nadhani sasa utaweza kutafuta thamani ya neno Hadiyd (الحديد Iron) yaani chuma.
 
Hadiyd Ili ni neno lenye herufi nne ambazo ni Ha, Da, Ya, na Da  na thamani yake kwa kila herufi ni kama ifuatavyo:   Ha = 8, Da = 4, Ya = 10, na Da = 4.


Na jumla ya thamani ya neno Hadiyd ni 26. Na ukianza kuhesabu kuanzia neno bismillahi mpaka kwenye aya yenyewe, inakuwa ni ya 26. Vile vile neno Allah (Mwenyezi Mungu) kuanzia mwanzo wa sura mpaka kwenye aya hii ya 25 neno Allah limetajwa mara 26. Aya 1, 5, 7, 8, 9, 11 15, 16, 17, 18, 22, 23 na 24 neno ili Allah limetajwa mara moja moja, na inafanya idadi kuwa mara 13. Katika aya ya 10 neno ili limetajwa mara 4, na aya ya 19, 20 na 25 limetajwa mara mbili mbili inafanya idadi kuwa mara 6, na aya ya 21, limetajwa mara tatu (3).
Ukijumlisha unapata 13+4+6+3 = 26.
 
Kimahesabu 26 ni atomic namba ya chuma (Fe). Yaani ni idadi ya protoni zilizoko katika chuma. Isitoshe pia sura hii imeitwa Al-Hadiyd katika kuitamka. Hapa zimeongezeka herufi mbili yaani, Alifu na Lam Ambazo thamani yake ni 31. kwa hiyo ukijumlisha na thamani ya neno Hadiyd  inakuwa  26+31 + 57. Kwa hiyo hapa neno Al-Hadiyd (الحديد) thamani yake itakuwa ni 57. Na kwa maajabu yake Mwenyezi Mungu sura hii imeiweka kuwa ya 57. Vile vile ukianzia kuhesabu mwisho wa msaafu kuelekea mwanzo inakuwa ni sura ya 58, nayo hii 58 ni Isotope namba ya kiatom ya chuma vievile.

No comments:

Post a Comment

Qur'an 5:32